Bilionea huyo amesema kuwa sheria hiyo ya kodi "inadhoofisha" juhudi za kupunguza matumizi za shirika lake la ufanisi.
Elon Musk ameonyesha kutoridhishwa na mswada mpya wa kodi na matumizi wa Rais wa Marekani, Donald Trump, akisema unadhoofisha juhudi za kupunguza deni la taifa.
Bunge la Wawakilishi limepitisha mswada huo unaolenga kuepuka ongezeko la kodi mwishoni mwa mwaka, lakini pia unaongeza deni la taifa ambalo sasa limefikia trilioni $36. Mswada huo sasa unasubiri kupigiwa kura na Seneti.
Musk, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla na SpaceX, na mmiliki wa X, amejiuzulu hivi karibuni kuongoza Idara ya Ufanisi wa Serikali (DOGE) — shirika lililoanzishwa na Trump katika muhula wake wa pili kwa ajili ya kupunguza matumizi ya serikali — ili arudi kuzingatia biashara zake.
Katika mahojiano na CBS, Musk alitoa ukosoaji wa nadra dhidi ya Trump, licha ya kuwa karibu naye katika wiki za mwanzo za muhula wake wa pili.
Elon Musk amesema amevunjika moyo na mswada mkubwa wa matumizi wa Trump uitwao "Big Beautiful Bill", akieleza kuwa unaongeza nakisi ya bajeti na kudhoofisha kazi ya Idara ya Ufanisi wa Serikali (DOGE) aliyokuwa akiiongoza.
Katika mahojiano, Musk alisema, “Muswada unaweza kuwa mkubwa au mzuri, lakini sidhani kama unaweza kuwa vyote viwili,” ikiwa ni ukosoaji wake mkali zaidi kwa sera za Trump hadi sasa.
Mswada huo unapendekeza kudumu kwa punguzo la kodi la mwaka 2017 na kuongeza matumizi katika ulinzi na usalama wa mipaka, huku wakosoaji wakisema unawafaidisha zaidi matajiri na unaweza kuongeza trilioni za deni la taifa katika muongo ujao.
Musk, ambaye alisaidia DOGE kuokoa dola bilioni 175 kupitia kufunga taasisi na kupunguza wafanyakazi, ana hofu kuwa mswada huo utapoteza mafanikio hayo.
Sasa mswada huo unaelekea Seneti, ambako unakabiliwa na upinzani kutoka kwa baadhi ya Warepublikani wanaohofia athari zake kwa bajeti ya taifa na huduma muhimu kama Medicaid na Medicare.
Comments
Post a Comment